NA SIMON CIURI
WANAWAKE watano na mtoto mmoja wameaga dunia baada ya simiti iliyokuwa imefunika kisima kuporomoka katika eneobunge la Ruiru, Kaunti ya Kiambu.
Simiti hiyo ilikuwa haijakauka vizuri.
Sita hao walikuwa wakisakata densi wakijiandaa kwa hafla ya harusi iliyofaa kufanyika leo Jumamosi asubuhi.
Mkasa umetokea nyumbani kwa Bwana Harusi katika eneo la Kihunguro.
Kamanda wa Polisi Kiambu, Perminus Kioi amethibitisha kwamba waliopoteza maisha ni wanawake watano na mtoto mmoja.
Aidha amesema majeruhi 11 wamepelekwa hospitalini baada ya kunasuliwa kutoka kwenye shimo hilo.