• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 8:50 AM
Wezi wavamia kanisa na kuiba mali yenye thamani ya Sh250,000

Wezi wavamia kanisa na kuiba mali yenye thamani ya Sh250,000

NA GEORGE MUNENE

WEZI wenye silaha walivamia kanisa la Katoliki la Christ The King Mukinduri Kaunti ya Kirinyaga na kuiba mali yenye thamani ya Sh250,000.

Kulingana na waumini, majambazi hao walivunja mlango wa kanisa Jumapili na kuiba kiibodi na bidhaa nyingine za kielektroniki.

“Tulipofika kanisani, tulipata dirisha limevunjwa na mlango kuharibiwa. Waliiba kiibodi na bidhaa nyingine za kielektroniki,” akasema Iren Wanjiru, mweka hazina wa kanisa hilo.

Muumini huyo alisema kuwa wezi hao pia walijaribu kuvamia makazi ya padre.

Mwenyekiti wa kanisa hilo, Peter Gikunju, aliomba polisi kufanya uchunguzi na kuwakamata wahalifu hao.

“Tunataka wezi hao wakamatwe na kama kanisa tupate mali yetu,” akasema Bw Gikunju.

  • Tags

You can share this post!

TUSIJE TUKASAHAU: Akiwa Waziri Mkuu Raila alishindwa...

Raila: Nimetamaushwa na mivutano ya ODM Kisii

T L