Na SHABAN MAKOKHA
FAMILIA zaidi ya 15,000 zinazoishi kwenye mpaka wa Uganda na Kenya Busia zitapata huduma ya maji safi baada ya mradi wa bwawa la maji la Angololo ulioanzishwa kati ya mataifa hayo mawili kukamilika.
Serikali za nchi hizo mbili zilishirikiana na zikaidhinisha ujenzi wa bwawa hilo kusaidia kunyunyuzia maji ekari zaidi ya 3,300 za mashamba.