• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 7:05 PM
Gavana Wanga alia kupokonywa mlinzi

Gavana Wanga alia kupokonywa mlinzi

NA GEORGE ODIWUOR

GAVANA wa Homa Bay Gladys Wanga anayataka mashirika yanayohusika na usalama wake kueleza ni kwa nini mlinzi wake aliondolewa wiki jana.

Gavana huyo ambaye ni miongoni mwa kundi la wanasiasa wanaoegemea muungano wa Azimio La Umoja – One Kenya Raila Odinga alisema hahisi salama baada ya mlinzi wake kuondolewa na serikali kwa sababu ambazo hakulezewa.

Bi Wanga, pamoja na Magavana wengine wa Nyanza Anyang Nyong’o (Kisumu), James Orengo (Siaya) na Ochilo Ayacko (Migori) walipokonywa walinzi wao wiki jana.

Hii ni baada ya kinara wa Azimio, Bw Raila Odinga kuitisha maandamano kuishinikiza serikali kupunguza gharama ya bidhaa za kimsingi.

Bi Wanga alisema kufikia sasa, hakuna maelezo yoyote ambayo yametolewa kwake kuhusu ni kwa nini mlinzi wake aliondolewa.

 

  • Tags

You can share this post!

Wanyonyi akung’uta Mandonga ‘Mtu Kazi’

Yaya aliyeangamiza afisa mkuu Kilifi alitoroshwa usiku kwa...

T L