NA PIUS MAUNDU
SHUGHULI za usafiri na uchukuzi katika barabara kuu ya Mombasa-Nairobi zimeathirika katika eneo la Sultan Hamud, Kaunti ya Makueni mnamo Jumanne baada ya Mto Sultan kuvunja kingo zake na maji ya mafuriko kutapakaa barabarani.
Hali hii imesababishwa na mvua kubwa iliyonyesha katika kaunti jirani ya Kajiado.
Wenye magari na pikipiki wanaonekana wakiwa waangalifu zaidi barabarani kufuatia hali hiyo.