NA MASHIRIKA
MFALME wa Uingereza Charles III amesema alihisi “uzito wa historia” na akaapa kufuata mfano uliowekwa na marehemu mama yake, Malkia Elizabeth II, katika hotuba yake ya kwanza kwa bunge Jumatatu.
“Ninaposimama mbele yenu leo, siwezi kujizuia kuhisi uzito wa historia ambayo inatuzunguka, na ambayo inatukumbusha mila muhimu ya bunge ambalo wajumbe wa mabunge yote mawili hujitolea kikamilifu kwa ajili ya maendeleo yetu sote. ” akasema.
Mfalme Charles alitamka hayo alpohutumbia mabunge ya House of Commons na House of Lords kwenye hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Westminster Hall, jengo kongwe zaidi katika eneo la bunge.