• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
Mfalme Charles III aahidi kufuata nyayo za mamake

Mfalme Charles III aahidi kufuata nyayo za mamake

NA MASHIRIKA

MFALME wa Uingereza Charles III amesema alihisi “uzito wa historia” na akaapa kufuata mfano uliowekwa na marehemu mama yake, Malkia Elizabeth II, katika hotuba yake ya kwanza kwa bunge Jumatatu.

“Ninaposimama mbele yenu leo, siwezi kujizuia kuhisi uzito wa historia ambayo inatuzunguka, na ambayo inatukumbusha mila muhimu ya bunge ambalo wajumbe wa mabunge yote mawili hujitolea kikamilifu kwa ajili ya maendeleo yetu sote. ” akasema.

Mfalme Charles alitamka hayo alpohutumbia mabunge ya House of Commons na House of Lords kwenye hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Westminster Hall, jengo kongwe zaidi katika eneo la bunge.

  • Tags

You can share this post!

Jeshi la Somalia laangamiza magaidi 100 wa Al-Shabaab

BIASHARA: Gharama ya juu yazima raha ya kilimo cha maua

T L