• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 3:24 PM
Wasafiri kutoka China kuzimwa

Wasafiri kutoka China kuzimwa

NA MASHIRIKA

RABAT, MOROCCO

MOROCCO imeweka marufuku dhidi ya wageni wanaoingia kutoka China, bila kujali uraia wao kuanzia Januari 3, kuzuia maambukizi ya corona, Wizara ya Masuala ya Kigeni imesema.

Nchi nyingi zimeweka vikwazo kwa wasafiri kutoka China kutokana na wimbi jipya la maambukizi ya Covid-19 linaloshuhudiwa nchini humo.

Maelfu ya watalii huzuru Morocco kutoka China kila mwaka, wanaosafiri kwa ndege zinazopitia eneo la Ghuba.

Mwezi huu wa Januari 2023, China ilianza kutekeleza mabadiliko katika sera ya kupambana na Covid-19 kwa kulegeza masharti ya kuzuia kusambaa kwa ugonjwa huo.

Masharti hayo ni kama vile marufuku dhidi ya watu kusafiri ndani na nje ya miji iliyoathirika na upimaji wa watu kwa wingi, hatua ambazo zinadaiwa kulenga kufufua uchumi wa China.

  • Tags

You can share this post!

Kundi la ADF lazidi kutisha, UG yakiri

Man-City wapoteza alama muhimu baada ya Everton...

T L