• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:01 AM
Avril achanganya mashabiki kwa kumsamehe J Blessing aliyedai alimpiga

Avril achanganya mashabiki kwa kumsamehe J Blessing aliyedai alimpiga

NA FRIDAH OKACHI

MWANAMUZIKI Avril Nyambura aomba mashabiki wake kumsamehe Produsa Jibril Blessing kwa tuhuma za kumchapa na kumsababishia majeraha usoni.

Mwanamuziki huyo amefuta akaunti yake ya Instagram, baada ya mashabiki kumshukia baada ya kumsamehe J Blessing ambaye wamekuwa naye kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka saba na kufanikiwa kuwa na mtoto mmoja.

Kabla hajafuta ukurasa wake, Avril alichukua fursa ya kusamehe produsa Blessing licha ya kumpa jeraha kwenye uso wake. Hali hii ikisababisha wawili hao kusabaratisha uhusiano wao.

Kwenye ukurasa wa Instagram, alichapisha msamaha huo, na kudai kuhitaji mabadiliko mapya.

“Moyo wangu una uzito wa kuelezea ulimwengu mambo yangu…Nimekusamehe J. Naomba mpate nafasi kwenye nyoyo zenu na kumsamehe pia. Kila mmoja anahitaji kusamehewa maishani,” aliandika Avril.

“Nimekuwa na uhusiano naye miaka 7 na safari ya kuwa wazazi kwa mtoto imekuwa sawa licha ya changamoto. Tumekuwa na mizozo kila wakati,” aliendelea.

Awali, Produsa J Blessing alikiri kuwepo na ugomvi uliomhusisha yeye na Avril bali alikana kumpiga na kueleza haungi mkono vurugu za kinyumbani.

Hii ni baada ya Avril kuchapisha picha za kutisha za uso zenye majeraha ya kushambuliwa.

“Habari za mchana. Ndiyo, tulikuwa na ugomvi hadharani, lakini haukuhusisha kumpiga kama ilivyofasiriwa. Siungi mkono aina yoyote ya vurugu,” alichapisha produsa J Blessing kwenye Instagram.

J Blessing alidai picha alizochapisha Avril ni tukio lililotokea mwaka jana.

Alikiri kuwa walikuwa na ugomvi uliosababisha kupigana, na kusababisha majeraha kwa wote wawili ambayo yalitibiwa hospitalini.

“Naomba radhi kwa madhara niliyomsababishia Avril au mtu mwingine yeyote. Nina hatia, lakini ningependa kufafanua mambo machache. Mwaka mmoja uliopita, tulikuwa na ugomvi wa kupigana sisi sote tulijeruhiwa, na nilimpeleka hospitali. Moja ya picha alizoweka ni tukio hilo,” J Blessing alisema.

“Jana usiku ugomvi ulitokea, lakini haikuwa jinsi anavyofasiriwa. Namhakikishia kila mtu kwamba sikumpiga Avril. Mimi sikumpiga. Mimi ni binadamu ambaye nilifanya makosa awali katika maisha yangu,” aliongeza produsa huyo.

J Blessings siku za hivi karibuni amekuwa akihusishwa kuwa na mahusiano na wanawake wengine watatu, kila mmoja akiwa na mtoto wake. Mahusiano ambayo yaliporomoka kwa njia ambayo haijulikani.

  • Tags

You can share this post!

Wakazi wa Molo wachoma maskani ya chang’aa wakiilaumu...

Bunge lakaidi mahakama na kuidhinisha polisi 1,000 watumwe...

T L