• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:01 AM
Diamond afunguka kuhusu madai ya kupunja wasanii wa Wasafi

Diamond afunguka kuhusu madai ya kupunja wasanii wa Wasafi

NA SINDA MATIKO

BAADA ya kumtambulisha msanii mpya, Diamond Platnumz sasa anasema yeye kuwasaini wasanii ni kuwafanyia hisani.

Wiki iliyopita, WCB inayomilikiwa na Diamond, ilimtangaza msanii wa singeli DVoice kuwa msanii mpya atakayekuwa chini ya lebo hiyo.

Akifunguka kuhusu kumsaini na sakata ambazo zimekuwepo za kuwa WCB inawanyonya wasanii, Diamond kafunguka na kusema biashara ya kusaini wasanii sio kitu kikubwa sana jinsi wengi wanavyodhania.

“Kama mikataba ni ya kinyonyaji mtu anafanikiwaje? Mbona wakitakiwa kulipa milioni mia tisa au bilioni moja ana uwezo wa kulipa. Ni kwa sababu mkataba unamnufaisha anapata mafanikio. Msanii unakuta Youtube yake kila mwezi inatengeneza sio chini ya milioni 48, unaniambiaje mimi niiache milioni 48 wakati nimewekeza kwake mamilioni ya fedha eti kwa sababu kajisikia aondoke. Sasa kama hela yangu ningeamua kuiweka kwenye kilimo, kwenye shamba ingekuwa tofauti,” Diamond anasema.

Staa huyo anasisitiza kuwa yeye kuwasaini wasanii WCB wala sio kazi ya kanisa.

“Hii ni biashara hakuna cha mtu kujitolea japokuwa nikikuchagua nitakuwa nimekusaidia maana nina zaidi ya watu mia wananiangalia Simba. Kwa hiyo nikikuchagua nimekufanyia hisani lakini pia tutakuwa tunafanya biashara, unapata na watu wanapata riziki,” ameongeza.

  • Tags

You can share this post!

Matineja waliopata mimba za mapema Kanduyi waingia ukahaba...

Nuru Okanga: Mfuasi sugu wa Raila bado hajapata matokeo ya...

T L