• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:55 AM
Mungai Eve, Trevor wanusurika kwenye ajali

Mungai Eve, Trevor wanusurika kwenye ajali

NA FRIDAH OKACHI

MTENGENEZAJI maudhui mwenye ufanisi mkubwa YouTube, Mungai Eve na mpenziwe Director Trevor, walinusurika bila majeraha katika ajali usiku wa kuamkia Krismasi.

Ujumbe ambao alipakia Desemba 26, 2023, kupitia ukurasa Instagram, mrembo huyo aliwashukuru mashabiki kwa kumjulia hali.

“Asanteni kwa kunijulia hali… niko sawa,” aliandika Eve.

Katika ujumbe mwingine, Eve aliandika kufahamisha mashabiki jinsi baadhi ya watu hukosa heshima baada ya ajali.

“Kuna ukosefu fulani wa heshima ambao kuomba msamaha au maelezo hayawezi kurekebisha,” akasema.

Hata hivyo, alichukua muda wake na kuwapa mashabiki hakikisho alikuwa mzima baada ya ajali iliyoacha gari lao la kwanza Toyota Crown likiwa limeharibika vibaya.

Toyota Crown KDG 373H lilikuwa gari la kwanza la Eve na mpenzi wake kununua kutokana na mapato ya YouTube kwa sababu kazi wanazofanya hutazamwa na mashabiki kibao.

Trevor aliandika baada ya ajali hiyo akisema ajali hiyo ilitokea kwenye barabara kuu.

Miongoni mwa video zilizosambazwa na Trevor, watu wa kwanza waliofika eneo la tukio kusaidia walisema gari hilo lilitoka nje ya barabara na kuingia kwenye mtaro baada ya kupata ajali kwenye sehemu ya lami iliyokarabatiwa siku chache zilizopita.

Trevor alichukua muda huo kumtafuta fundi wa gari almaarufu mekanika maarufu kutoka mjini Nairobi kuwasaidia kusanya mabaki ya gari.

Mwaka 2022, Trevor aliandika kwenye ukurasa wa Instagram kuhusu kununua gari lao kwanza.

“Kutana na mtoto wetu wa kwanza, tulifanya hivyo mpenzi wangu. Namshukuru Mungu kwa umbali aliotufikisha. Sikujua kwa wakati huu tungekuwa hapa lakini kwa neema na rehema zake tumefanikiwa! Siamini hatimaye kumiliki gari kutokana na fadhila za Mwenyezi Mungu kwa kwa kutujalia ushindi mwingi zaidi pamoja hunny na kumbuka kila wakati tuko ndani yake kushinda!” aliandika Trevor.

  • Tags

You can share this post!

Usifakamie mlo tu kujaza tumbo – mtaalamu

Mlipuko wa meli watikisa Mombasa

T L