• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 5:29 PM
Jinsi ya kuandaa kamba kwa kukaanga

Jinsi ya kuandaa kamba kwa kukaanga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 20

Muda wa mapishi: Dakika 10

Walaji: 4

Vinavyohitajika

kamba kilo 1

pilipili iliyotwangwa kijiko 1

ndimu iliyokamuliwa vijiko vikubwa 2

chumvi

kitunguu saumu kilichotwangwa kiasi cha kijiko 1

chicken masala (au masala yoyote) kijiko 1

mafuta ya kupikia

maji kiasi kwa ajili ya kuoshea kamba

Maelekezo

Osha kamba vizuri kisha waweke kwenye bakuli kubwa kiasi.

Waweke vitu vyote nilivyotaja hapo juu kasoro mafuta.

Vaa glavu mkononi halafu changanya vizuri mpaka kamba wakolee viungo kisha waache kwa dakika 10 waingie viungo vizuri.

Mimina mafuta kwenye kikaangio halafu weka mekoni kikaangio kipate moto vizuri.

Weka kamba na bila shaka utawaona wanabadilika rangi na kuonekana wakiwa na rangi ya dhahabu.

Kamba. PICHA | MARGARET MAINA

Waache kwa dakika tatu tu kisha wageuze kwa kuwachanganya.

Subiri kwa muda wa dakika tatu nyingine halafu waepue na uweke kwenye chujio wachuje mafuta.

Subiri chakula chako kipoe. Unaweza ukala kamba tu au ukala kamba pamoja na wali, mkate na kadhalika

  • Tags

You can share this post!

Fainali za mashindano ya michezo ya vyuo vya kiufundi...

Shujaa yatiwa kundi moja na Amerika ya Mike duru ya Dubai...

T L