NA MERCY KOSKEI
NDOA ya mwanahabari Kamene Goro ipo kwenye mizani baada ya mumewe ambaye ni mcheza santuri, DJ Bonez, kukiri kwamba hawezi kamwe kumpigania.
Ufichuzi huu ulijidhihirisha kupiitia kipindi cha kuvutia YouTube, ambapo mtangazaji huyo wa zamani wa redio aliuliza swali ikiwa Bonez angejitokeza na kumpigania.
“Kwa hivyo ikiwa mtu atanigusa makalio yangu, utanipigania? Kwa hivyo huwezi kunipigania? Huwezi kunipigania?” Kamene alisikika akiuliza kwa sauti ya mchanganyiko wa kukata tamaa na kutoamini.
Bonez alipojibu, “Siwezi kupigana na mwanamume,” kuchanganyikiwa kwa Kamene kulizidi kwani hakuweza kufahamu kwamba baada ya ndoa, angedai ghafla kutokuwa na uwezo wa kumpigania.
Hata hivyo, DJ Bonez alionekana kutoshtushwa na dhiki yake na akapuuza wazo la kupigana na kupendekeza kwamba mapigano yanapaswa kutengwa kwa ajili ya bondia wa zamani Mike Tyson.
Jibu hilo la kustaajabisha lilimtia hasira zaidi Kamene, na kumfanya apendekeze kuwa kipindi kiishe.
Kwa sauti ya kuchanganyikiwa na isiyo na matumaini, alionyesha kusikitishwa kwake na DJ Bonez, akihisi kana kwamba alikuwa amebadilika.
Mcheshi Oga Obinna, wamekuwa wakiburudisha watazamaji kupitia podikasti zao za kila wiki kwenye chaneli ya Kamene na Obinna.
Hata hivyo, ugomvi huu wa hivi majuzi ulifichua mpasuko katika uhusiano wa Kamene na Bonez, na kuongeza safu ya mvutano baina yao.