• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 1:13 PM
Mamake Trio Mio aomba msaada wa DCI mwanawe akitishwa kuuawa

Mamake Trio Mio aomba msaada wa DCI mwanawe akitishwa kuuawa

NA MERCY KOSKEI

IRMA Sakwa, mama na meneja wa mwimbaji maarufu Trio Mio, ameibua wasiwasi kuhusu usalama wa mwanawe kufuatia vitisho vya kifo vilivyochapishwa mtandaoni.

Hii ni baada ya mtumiaji wa Twitter aliyetambulika kama Theecarbon4, kusambaza ujumbe ambapo wanaume wawili walisikika wakitema vitisho vya kifo kwa Trio Mio wakidai kuwa alitoroka na pesa zao.

“Trio Mio, kwa nini uliiba pesa zetu? Tutakumaliza. Hatuna hofu,” unasema ujumbe uliochapishwa Mei 31, 2023.

Hii imemlazimu mamake Trio Mio kuomba msaada kutoka kwa Idara ya Upelelezi ya Jinai (DCI) kumlinda mtoto wake dhidi ya vitisho hivyo hatari.

“Hili si jambo la kuchekesha hata kidogo. Si kitambo, mwanangu aliibiwa na wahuni waliokua wamejihami na bunduki; bado hatujamaliza kiwewe. Kisha hii? DCI, mmeona hii? Mimi kama mzazi naomba kwa unyenyekevu hatua ichukuliwe dhidi ya wahusika hawa! Moyo wangu hauna amani. Mungu amlinde mtoto wangu,” aliandika.

Kufikia sasa DCI bado haijatoa mwelekeo licha ya video hiyo kuwa ingali kwenye mitandao.

Aprili 2023, Trio Mio alifichua kwamba alipoteza simu zake mbili na funguo za gari kwa watu watatu waliompora huku wakitishia kumpiga risasi.

Kulingana na Trio Mio, wakati wa tukio alikuwa akirejea nyumbani kutoka studio.

Inasemekana kuwa majambazi hao walimtambua mwanamuziki huyo na kumsalimia kabla ya kuingia kwenye gari lake wakiwa na bunduki na mwingine panga.

“Nilikuwa tayari kuwapa kila kitu, viatu na nguo zangu ilimradi niokoe maisha yangu. Walikuwa wameikoki bunduki na kuiweka juu ya tumbo langu. Walichukua simu zangu mbili na nikawapa funguo za gari,” alisimulia.

 

  • Tags

You can share this post!

Wahuni waliopora wanandoa wa China mamilioni Juja wasakwa  

Ole wenu vidosho mliommezea mate mtangazaji Hassan Mugambi,...

T L