• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
Ole wenu vidosho mliommezea mate mtangazaji Hassan Mugambi, amenyakuliwa

Ole wenu vidosho mliommezea mate mtangazaji Hassan Mugambi, amenyakuliwa

NA MERCY KOSKEI

MTANGAZAJI wa runinga ya Citizen Hassan Mugambi amefunga pingu za maisha na mpenzi wake wa siku nyingi Mwanaidi Shishi katika sherehe ya Kislaamu, Nikah.

Sherehe hiyo ya faragha ilifanyika Ijumaa, Juni 9, 2023 na Jumamosi, Juni 10 katika Msikiti wa Makina Kibra, Nairobi na ilihudhuriwa na familia na marafiki wa karibu.

Mfanyakazi mwenza Rashid Abdalla, kupitia kwa mtandao wake wa Instagram alisambaza picha ya wanandoa hao, huku akiwatakia baraka zaidi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Picha hiyo ilinasa Mugambi, Rashid Abdalla, Ayub Abdikadir, na mbunge wa Mugirango Kusini Silvanus Osoro.

Bw Osoro ambaye pia ni kiranja wa wengi bunge la kitaifa, alichapisha na kupakia picha za harusi ya Bw Mugambi mitandaoni.

Mwanahabari huyo mpelelezi alivalia mavazi ya harusi ya Kiislamu, ikiwa ni pamoja na kanzu ya bluu na kofia inayofanana.

Abdikadir aliwatakia wanandoa hao baraka katika safari yao ya ndoa.

“Mwenyezi Mungu akuongoze Hassan Mugambi unapoingia kwenye mkataba mzito siku ya harusi yako,” alisema.

Mwanaidi ni mfanyabiashara ambaye kwa sasa anamiliki mkahawa unaoitwa Mama Nilishe, ulioko mtaa wa kifahari wa Kilimani na upika vyakula vya Uswahilini.

Mugambi alianza kazi yake ya uanahabari Pamoja FM, kituo cha redio cha kijamii Kibera.

Alitumia jukwaa hilo kukuza na kupalilia ufasaha wake katika lugha ya Kiswahili.

Baadaye, aliajiriwa na K24 TV, ambapo alifanya kazi kwa miaka mitano kabla ya kujiunga na Citizen TV 2017.

Wakenya pia hawakuwachwa nyuma, kwani wengine waliwatakia heri njema katika ndoa yao.

 

 

  • Tags

You can share this post!

Mamake Trio Mio aomba msaada wa DCI mwanawe akitishwa kuuawa

Wabunge Tharaka Nithi: Waziri Kindiki ametosha mboga...

T L