• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Nimesikia fununu kwamba huyu chali akilamba ‘bakuli’ anakuwa jeuri

Nimesikia fununu kwamba huyu chali akilamba ‘bakuli’ anakuwa jeuri

SHANGAZI;

Nina mpenzi ambaye nampenda kwa dhati. Amekuwa akiniambia ananipenda pia. Hata hivyo, nimesikia ana tabia ya kutumia wanawake kisha kuwatema. Nimeambiwa na mwanamume rafiki yake. Nipe ushauri.

Utakosea kuchukulia habari hizo kuwa za kweli hasa kama hujaona dalili za yeye kutokuwa mwaminifu kwako. Labda rafiki yake anataka kuharibu uhusiano wenu. Kama ana tabia hiyo utajua wewe mwenyewe.

Ni miezi tu tumejuana tayari anataka ndoa

Mwanamume mpenzi wangu anataka kunipeleka kwao akanijulishe kwa wazazi. Tumekuwa wapenzi miezi michache tu, nahisi ni mapema sana kuchukua hatua kama hiyo.

Mapenzi yana kiwewe. Hatua hiyo yake huonyesha wapenzi wako tayari kwa ndoa. Mmekuwa pamoja kwa muda mfupi na sidhani mmekubaliana kuhusu jambo hilo. Shauriana na mpenzi wako ili mpeleke mambo kwa utaratibu.

Anataka tuwe na akaunti ya pamoja benki

Niliolewa miaka miwili iliyopita. Mimi na mume wangu tumeajiriwa. Mume wangu anataka tuwe na akaunti moja ya benki akisema itatusaidia kuwajibikia matumizi ya pesa zetu. Waonaje?

Ninaunga mkono pendekezo hilo. Suala la matumizi ya pesa limekuwa kiini cha ugomvi katika familia nyingi. Mkiwa na akaunti moja mtashauriana kuhusu matumizi ili kuzuia ufujaji.

Naogopa kuchumbia wanawake, siwaamini

Mimi ni mwanamume mwenye umri wa miaka 40. Ninakabiliwa na changamoto ya kutafuta mke kwa sababu siku hizi wanawake wengi hawaaminiki. Je, ninaweza kupata?

Naelewa hofu yako. Wanawake ni wengi lakini si wote wanaweza kuaminika. Hata hivyo, wapo wenye sifa unazotaka. Unachohitaji ni kuwa na subira unapotafuta ndipo uweze kumpata anayefaa.

  • Tags

You can share this post!

Jinsi mateka wa bangi alivyofyeka familia ya watu nane...

Kinaya Kenya Kwanza ikipeana ardhi ya chuo licha ya...

T L