NA MWORIA MUCHINA
MJUSI anayeitwa thorny devil hunywa maji kupitia miguu na ngozi.
Anapatikana jangwani na alipata jina yake kutokana na pembe zilizoko kichwani ambazo humfanya afanane na shetani.
Ngozi yake yenye miiba humsaidia kuepuka maadui kwa vile hakuna kiumbe anayeweza kummeza mjusi huyu.
Pia, ana mkia unaofanana na kichwa na anapovamiwa huficha kichwa chake katikati ya miguu na kuacha mkia kuonekana kama ndio kichwa.
Hula wadudu kama siafu na mchwa na kwa vile mdomo wake hauwezi kunywa na kumeza maji, mjusi huyu huonekana amejitandaza wakati wa mvua au huingia kwenye vidimbwi vya maji kusudi ngozi yake iloe maji ambayo hatimaye huingia mwilini.