Mpendwa Daktari,
Ningependa kujua mengi kuhusu ishara za kansa ya ulimi.
Jason, Mombasa
Mpendwa Jason,
Kansa ya ulimi hutokana na uvimbe unaoanza kujitokeza kwenye sehemu ya ulimi au nyuma ya koo.
Ishara za kansa ya ulimi
Masuala yanayoongeza hatari ya kukumbwa na kansa ya ulimi?
Matumizi ya tumbaku: Watu wanaotumia bidhaa za tumbaku kama vile sigara, wako katika hatari kubwa ya kukumbwa na maradhi haya.
Unywaji pombe: Pombe inasemekana kusababisha sio tu kansa ya ulimi bali pia aina zingine za kansa za mdomoni.
Kuwahi pitishwa kwenye miali ya mwanga: Iwapo uliwahi ugua aina ingine ya kansa kama vile ya kichwa au ya shingo, iliyokulazimu kupokea matibabu kwa miali ya mwanga, basi una uwezekano mkubwa wa kukumbwa na kansa ya mdomoni.
Kutozingatia lishe bora: Kutokula mboga na matunda kwa wingi, kunaongeza hatari ya kukumbwa na aina hii ya kansa.
Maambukizi ya virusi vya human papillomavirus HPV: Virusi hivi pia vimetambulika kama mojawapo ya vichocheo vya sio tu kansa ya mdomoni bali pia ya njia ya uzazi.
Unashauriwa kumuona daktari iwapo utashuhudia ishara za aina hii kwani aina hii ya kansa husambaa upesi katika sehemu zingine za mdomo kama vile ufizi, taya na koo.