• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 6:07 PM
Arsenal kuvunja benki ili kusajili kiungo James Maddison

Arsenal kuvunja benki ili kusajili kiungo James Maddison

Na MASHIRIKA

ARSENAL wako radhi kutoa Sh9.3 bilioni pamoja na mchezaji mmoja kati ya Ainsley Maitland-Niles, Joe Willock, Reiss Nelson na Eddie Nketiah ili kushawishi Leiceter City kumwachilia kiungo James Maddison atue uwanjani Emirates.

Kocha Mikel Arteta amekuwa akimezea mate maarifa ya Maddison, 24, kwa muda mrefu na kinachomchochea kuwania huduma zake ni haja ya kutafuta kiungo mbunifu atakayeshirikiana vilivyo na mafowadi wake tangu Mesut Ozil aondoke kambini mwa Arsenal.

Arsenal wanaanza kuhemea Maddison baada ya matumaini ya kumdumisha kiungo wa Real Madrid, Martin Odegaard aliyewachezea kwa mkopo mnamo 2020-21 kudidimia.

Odegaard ambaye ni raia wa Norway, tayari amerejea jijini Madrid, Uhispania kuungana na wachezaji wenzake uwanjani Santiago Bernabeu chini ya kocha mpya, Carlo Ancelotti aliyeagana na Everton mwishoni mwa msimu wa 2020-21.

Maddison amewahi pia kuchezea Norwich City na Coventry.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Amerika yapepeta Mexico na kutwaa taji la Concacaf Gold Cup

Brazil kukutana na Uhispania kwenye fainali Olimpiki