• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Barcelona washuka zaidi ligini baada ya kukabwa koo na Osasuna

Barcelona washuka zaidi ligini baada ya kukabwa koo na Osasuna

Na MASHIRIKA

MASAIBU ya Barcelona katika kampeni za msimu huu yaliendelezwa na Osasuna waliowalazimishia sare ya 2-2 kwenye Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumapili.

Matokeo hayo yaliteremsha Barcelona hadi nafasi ya nane kwenye msimamo wa jedwali la La Liga kwa alama 15 zaidi nyuma ya viongozi Real Madrid.

Matineja Nicolas Gonzalez na Abdessamad Ezzalzouli walio na umri wa miaka 19 kila mmoja ndio waliofuma wavuni mabao ya Barcelona waliokuwa wakichezea ugenini.

Wafungaji kwa upande wa Osasuna walikuwa wanasoka David Garcia na Ezequiel Avila.

Barcelona walishuka dimbani wakiwa na ulazima wa kusajili ushindi baada ya chombo chao kuzamishwa awali na Real Betis na Bayern Munich katika La Liga na Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) mtawalia.

Huku Barcelona wakijivunia sasa alama 24 kutokana na mechi 16 zilizopita ligini, Osasuna wanakamata nambari ya 10 kwa pointi 22 baada ya kutandaza jumla ya michuano 22.

MATOKEO YA LA LIGA (Jumapili):

Osasuna 2-2 Barcelona

Real Madrid 2-0 Atletico

Villarreal 2-0 Vallecano

Real Betis 4-0 Sociedad

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Rangers kumenyana na Dortmund kwenye mchujo wa Europa League

Mbappe aongoza PSG kuzamisha Monaco ligini

T L