• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Beki Axel Tuanzebe ajiunga na Napoli ya Italia kwa mkopo

Beki Axel Tuanzebe ajiunga na Napoli ya Italia kwa mkopo

Na MASHIRIKA

BEKI wa Manchester United, Axel Tuanzebe amejiunga na Napoli ya Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mkopo wa hadi mwisho wa msimu huu wa 2021-22.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 alirejea ugani Old Trafford mwanzoni mwa Januari 2022 baada ya kukosa nafasi ya kuunga kikosi cha kwanza cha Aston Villa alikokuwa akicheza kwa mkopo chini ya kocha Steven Gerrard.

Tuanzebe aliingia katika sajili rasmi ya Man-United na umri wa miaka minane na amechezea kikosi hicho mara 37 tangu awajibishwe katika kikosi cha kwanza mnamo 2017. Villa walimchezesha mara 45 katika kipindi cha misimu mitatu ya mkopo kambini mwao.

Kufikia sasa, Napoli wanakamata nafasi ya tatu kwenye msimamo wa jedwali la Serie A nyuma ya Inter Milan na AC Milan na wameratibiwa kupambana na Barcelona katika mchujo wa kuingia Europa League mnamo Februari 2022. Tuanzebe aliondoka mjini Bunia nchini DR Congo akiwa mtoto mdogo kuelekea Uingereza kujikuza katika ulingo wa soka.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

MWALIMU WA WIKI: Anatumia nyimbo kufunzia darasani

TAHARIRI: Kuhubiri chuki ya kisiasa tishio kwa taifa kabla...

T L