• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 9:35 PM
Brentford yazamisha chombo cha West Ham United ligini

Brentford yazamisha chombo cha West Ham United ligini

Na MASHIRIKA

MATUMAINI ya West Ham United kukamilisha kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) ndani ya orodha ya nne-bora msimu huu yalififishwa na Brentford waliowakung’uta 2-0 mnamo Jumapili.

Mabao ya Brentford yalijazwa kimiani kupitia Bryan Mbeumo na Ivan Toney. Chini ya kocha Thomas Frank, kikosi hicho kilipaa hadi nafasi ya 13 jedwalini kwa alama 36 sawa na Aston Villa na Southampton.

Ni pengo la alama 12 sasa ambalo linawatenganisha na Burnley ambao kwa pamoja na Watford na Norwich City, wanakodolea macho hatari ya kuteremshwa ngazi ligini mwishoni mwa msimu huu.

Kichapo kutoka kwa Brentford kiliwashusha West Ham wanaonolewa na kocha David Moyes hadi nafasi ya sita jedalini kwa alama 51 sawa na nambari saba Manchester United. Hofu zaidi kwa West Ham ni kwamba wamesakata jumla ya michuano 32, moja zaidi kuliko Man-United. Arsenal wanakamata nafasi ya tano kwa alama 54, tatu nyuma ya Tottenham Hotspur wanaofunga orodha ya nne-bora.

Pigo zaidi kwa West Ham ni jeraha la kifundo cha mguu ambalo sasa litamweka nje beki Kurt Zouma kadri wanavyojiandaa kurudiana na Olympique Lyon ya Ufaransa katika robo-fainali ya Europa League mnamo Aprili 14, 2022 nchini Ufaransa. West Ham waliambulia sare ya 1-1 dhidi ya Lyon katika mkondo wa kwanza ugani London Stadium mnamo Aprili 7, 2022.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Jubilee njiapanda maelewano kati ya wawaniaji yakifeli

Maafande wa Kenya Police wazima MSC

T L