• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 8:55 PM
De Bruyne, Foden kutochezea Man-City dhidi ya Spurs

De Bruyne, Foden kutochezea Man-City dhidi ya Spurs

Na MASHIRIKA

KIUNGO Kevin de Bruyne wa Ubelgiji atakosa mchuano wa ufunguzi wa kampeni za Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu utakaokutanisha waajiri wake Manchester City na Tottenham Hotspur leo Jumapili.

De Bruyne, 30, bado hajarejelea mazoezi mazito kambini mwa Man-City tangu apate jeraha la kifundo cha mguu wakati wa fainali za Euro 2020.

“Anaimarika siku baada ya nyingine ila bado tunasubiri tathmini ya daktari wake. Hata hivyo, dalili zote zinaashiria kwamba hatakuwa sehemu ya kikosi tutakachotegemea dhidi ya Spurs,” akasema kocha Pep Guardiola.

De Bruyne aliibuka mshindi wa taji la Mchezaji Bora wa Muungano wa Wanasoka Wataalamu (PFA) mnamo 2020-21 kwa mara ya pili mfululizo baada ya kusaidia Man-City kutwaa taji la tatu la EPL chini ya kipindi cha miaka minne.

Phil Foden ambaye pia alishinda taji la Chipukizi Bora wa PFA mnamo 2020-21, atakosa mechi dhidi ya Spurs kutokana na jeraha la mguu.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Wakala wa Lukaku atishiwa maisha kwa kufanikisha uhamisho...

DINI: Lisheni akili zenu mawazo mazuri, fikra za tumaini na...