• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 3:24 PM
Dortmund na Bayern watamba katika michuano yao ya Bundesliga

Dortmund na Bayern watamba katika michuano yao ya Bundesliga

Na MASHIRIKA

KIUNGO mvamizi raia wa Uingereza, Jude Bellingham, alifunga mabao mawili na kusaidia waajiri wake Borussia Dortmund kupepeta Stuttgart 5-0 katika ushindi uliowapaisha hadi ndani ya mduara wa tano-bora katika Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga).

Dortmund walianza mechi kwa kasi ya juu na wakawa wanajivunia uongozi wa 3-0 kufikia mwisho wa kipindi cha kwanza baada ya kufungiwa mabao na Bellingham, Niklas Sule na Giovanni Reyna. Bellingham alipachika wavuni bao lake la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili kabla ya Dortmund kupata goli la tano kupitia kwa Youssoufa Moukoko.

Bayern Munich walipokeza Hoffenheim kichapo cha 2-0 na kupaa hadi nafasi ya pili kwa alama 22, moja pekee nyuma ya viongozi Union Berlin ambao wana mchuano wa ziada.

Ilikuwa mara ya kwanza tangu Agosti 2022 kwa Bayern ambao ni mabingwa watetezi wa Bundesliga kushinda michuano miwili mfululizo kwenye kampeni za muhula huu wa 2022-23.

Miamba hao wanaonolewa na kocha Julian Nagelsmann walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Jamal Musiala aliyeshirikiana vilivyo na Leon Goretzka. Eric Maxim Choupo-Moting alifungia Bayern bao la pili baada ya kumegewa krosi safi na Serge Gnabry.

MATOKEO YA BUNDESLIGA (Jumamosi):

Dortmund 5-0 Stuttgart

Hoffenheim 0-2 Bayern

Leverkusen 2-2 Wolfsburg

Augsburg 3-3 RB Leipzig

Freiburg 2-0 Werder Bremen

M’gladbach 1-3 Frankfurt

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Real Madrid wakomoa Sevilla na kufungua pengo la alama sita...

TAHARIRI: Mageuzi katika polisi yasiingizwe siasa

T L