• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 1:22 PM
Real Madrid wakomoa Sevilla na kufungua pengo la alama sita kileleni mwa jedwali la La Liga

Real Madrid wakomoa Sevilla na kufungua pengo la alama sita kileleni mwa jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

REAL MADRID walifungua mwanya wa alama sita kileleni mwa jedwali la Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) baada ya kupepeta Sevilla 3-1 mnamo Jumamosi ugani Santiago.

Mabingwa hao watetezi walifungua ukurasa wa mabao kupitia kwa Luka Modric kunako dakika ya tano kabla ya Erik Lamela kusawazisha mambo katika dakika ya 54.

Ililazimu Real kusubiri hadi mwishoni mwa kipindi cha pili kufungiwa mabao mawili ya haraka kupitia kwa Lucas Vazquez na Fede Valverde na kujitwalia ushindi uliowadumisha kileleni mwa jedwali kwa alama 31. Barcelona wanakamata nafasi ya pili japo wana mchuano wa ziada dhidi ya Athletic Bilbao mnamo Oktoba 23, 2022 ugani Camp Nou.

Mechi dhidi ya Sevilla ilikuwa ya 10 kati ya 11 zilizopita  wa Real ya kocha Carlo Ancelotti kushinda katika kampeni za La Liga msimu huu.

Bao la Vazquez lilikuwa zao la ushirikiano mkubwa kati yake na Marco Asensio aliyeingia uwanjani katika kipindi cha pili.

Japo wamekuwa wakisuasua msimu huu, kichapo kutoka kwa Real kilikuwa cha kwanza kwa kocha mpya wa Sevilla, Jorge Sampaoli, kupokea baada ya kusimamia michuano mitano tangu aaminiwe kuwa mrithi wa Julen Lopetegui. Matokeo hayo yalisaza Sevilla katika nafasi ya 14 jedwalini kwa alama 10 sawa na Almeria na Celta Vigo.

MATOKEO YA LA LIGA (Jumamosi):

Real Madrid 3-1 Sevilla

Rayo Vallecano 5-1 Cadiz

Valladolid 1-0 Real Sociedad

Valencia 1-2 Mallorca

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

KIGODA CHA PWANI: Wapigakura watarajia makuu kwa...

Dortmund na Bayern watamba katika michuano yao ya Bundesliga

T L