• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 3:09 PM
Haaland awabeba Dortmund dhidi ya Furth ligini

Haaland awabeba Dortmund dhidi ya Furth ligini

Na MASHIRIKA

ERLING Braut Haaland alifunga mabao mawili na kusaidia waajiri wake Borussia Dortmund kukomoa Greuther Furth 3-0 katika mchuano wa Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) mnamo Jumatano usiku.

Haaland, 21, aliwaweka Dortmund kifua mbele kupitia penalti ya dakika ya 33 kabla ya kukamilisha frikiki ya Julian Brandt mwishoni mwa kipindi cha pili. Nyota huyo raia wa Norway sasa anajivunia mabao 19 kutokana na mechi 15 msimu huu.

Brandt alichangia pia bao la tatu ambalo Dortmund walifungiwa na Donyell Malen katika dakika ya 89. Kufikia sasa, Dortmund wanashikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa jedwali la Bundesliga kwa alama 34, sita zaidi nyuma ya viongozi na mabingwa watetezi Bayern Munich.

Chini ya kocha Marco Rose, Dortmund pia wanajivunia pengo la alama sita kati yao na nambari tatu Bayer Leverkusen waliolazimishiwa sare ya 2-2 dhidi ya Hoffenheim nyumbani.

Dortmund watakuwa wageni wa Hertha Berlin katika mchuano wao ujao ligini mnamo Disemba 18, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Arsenal wakomoa West Ham United na kuingia nne-bora EPL

VYAMA: Kongamano la sita la CHAUKIDU laanza rasmi katika...

T L