• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Impala yaendea Mwamba fainali ya Ligi Kuu ya raga ya kinadada

Impala yaendea Mwamba fainali ya Ligi Kuu ya raga ya kinadada

Na GEOFFREY ANENE

Mbivu na mbichi kuhusu nani mkali katika Ligi Kuu ya raga ya wanawake nchini (Kenya Cup) itajulikana wakati wenyeji Impala watavaana na Mwamba saa kumi jioni leo Jumamosi.

Impala, ambao walishinda msimu wa kawaida, wanapigiwa upatu. Kocha Mary Ochieng’ anajivunia kuwa na wachezaji matata kama Christabel Lindo, Stella Wafula na Leah Wambui.

Mwamba ya kocha Baabu Odindo ina mtimkaji hodari Janet Okello pamoja na Sarah Oluche na Terry Ayesa. Impala ililima Northern Suburbs 17-7 katika nusu-fainali nayo Mwamba ikabandua Top Fry Nakuru 36-6.

Mechi hiyo itatanguliwa na wanafainali wa Kenya Cup ya wanaume Menengai Oilers dhidi ya Impala Saracens katika raundi ya 16-bora ya Kombe la Enterprise. Oilers walipoteza fainali ya ligi ya wanaume dhidi ya wanasukari wa Kabras Sugar mjini Kakamega wikendi iliyopita.

You can share this post!

Lewandowski aweka rekodi mpya ya ufungaji wa mabao...

Unavyoweza kufanikisha ufugaji wa nguruwe jijini

T L