• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 5:55 AM
Kasikasi FC, Kisa FC na Melta Kabiriah Youth ndio mabingwa wa kategoria mbalimbali za Ligi FKF

Kasikasi FC, Kisa FC na Melta Kabiriah Youth ndio mabingwa wa kategoria mbalimbali za Ligi FKF

NA PATRICK KILAVUKA

KASIKASI FC, Kisa FC na Melta Kabiria Youth ndio mabingwa wa Ligi ya Kanda, Kaunti na Kaunti Ndogo, FKF Nairobi West mtawalia kwa upande wa wanaume katika mikwaruzano ya mchujo kutafuta mabingwa viwango hivyo iliyoandaliwa katika uga wa Kihumbuini mnamo Jumapili.

Kasikasi walikabiliana na Simba United katika mchujo wa mabingwa wa Ligi ya Kanda na kuwanyamazishwa matuta 5-3 baada ya kuambulia sare tasa katika muda wa kawaida.

Kisa walitawazwa mabingwa wa Ligi ya Kaunti baada ya kufyeka Nkoroi 4-2 na Kibagare Sportiff 3-2.

Kikosi cha Kisa FC. PICHA | PATRICK KILAVUKA

Melta Kabiriah Youth nayo ilipepeta Royal Soccer 4-1 na South B Wazito 4-2 na kukusanya alama sita muhimu.

Timu zote zilipanda madaraja ya juu na kutuzwa medali na vikombe.

  • Tags

You can share this post!

MUME KIGONGO: Usipolala vizuri mbegu za kiume zitapungua

TALANTA: Dogo anayetamba katika muziki wa ala na sarakasi

T L