NA PATRICK KILAVUKA
KASIKASI FC, Kisa FC na Melta Kabiria Youth ndio mabingwa wa Ligi ya Kanda, Kaunti na Kaunti Ndogo, FKF Nairobi West mtawalia kwa upande wa wanaume katika mikwaruzano ya mchujo kutafuta mabingwa viwango hivyo iliyoandaliwa katika uga wa Kihumbuini mnamo Jumapili.
Kasikasi walikabiliana na Simba United katika mchujo wa mabingwa wa Ligi ya Kanda na kuwanyamazishwa matuta 5-3 baada ya kuambulia sare tasa katika muda wa kawaida.
Kisa walitawazwa mabingwa wa Ligi ya Kaunti baada ya kufyeka Nkoroi 4-2 na Kibagare Sportiff 3-2.
Melta Kabiriah Youth nayo ilipepeta Royal Soccer 4-1 na South B Wazito 4-2 na kukusanya alama sita muhimu.
Timu zote zilipanda madaraja ya juu na kutuzwa medali na vikombe.