Na MASHIRIKA
MANCHESTER United watakutana na Barcelona kwenye mchujo wa mikondo miwili kuingia raundi ya 16-bora ya Europa League msimu huu.
Hatua hiyo ya muondoano inahusisha klabu nane zilizoambulia nafasi ya pili kwenye makundi ya Europa League, ikiwemo Man-United, ambazo zitakachuana na vikosi vilivyokamilisha kampeni ya makundi ya UEFA katika nambari ya tatu.
Mechi za mkondo wa kwanza katika mchujo huo zitatandazwa Februari 16, 2023 kabla ya marudiano kufanyika wiki moja baadaye. Man-United watatangulia kutua ugani Camp Nou kabla ya kualika Barcelona uwanjani Old Trafford.
Chini ya kocha Erik ten Hag, Man-United waliambulia nafasi ya pili nyuma ya Real Sociedad katika Kundi E la Europa League huku Barcelona wakiridhika na nafasi ya tatu nyuma ya Inter Milan na Bayern Munich katika Kundi C la UEFA.
Jose Mourinho ataongoza waajiri wake AS Roma kuchuana na FC Salzburg huku Sporting Lisbon wakimenyana na Midtjylland. Shakhtar Donetsk watakwaruzana na Rennes, Ajax waonane na Union Berlin nao Leverkusen wapambane na AS Monaco. Sevilla watakabiliana na PSV Eindhoven.
Barcelona vs Man-United
Juventus vs Nantes
Sporting vs Midtjylland
Shakhtar Donetsk vs Rennes
Ajax vs Union Berlin
Leverkusen vs Monaco
Sevilla vs PSV Eindhoven
FC Salzburg vs Roma
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO