• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 8:57 PM
Man-United kuvaana na Barcelona katika mchujo wa kuingia hatua ya 16-bora ya Europa League

Man-United kuvaana na Barcelona katika mchujo wa kuingia hatua ya 16-bora ya Europa League

Na MASHIRIKA

MANCHESTER United watakutana na Barcelona kwenye mchujo wa mikondo miwili kuingia raundi ya 16-bora ya Europa League msimu huu.

Hatua hiyo ya muondoano inahusisha klabu nane zilizoambulia nafasi ya pili kwenye makundi ya Europa League, ikiwemo Man-United, ambazo zitakachuana na vikosi vilivyokamilisha kampeni ya makundi ya UEFA katika nambari ya tatu.

Mechi za mkondo wa kwanza katika mchujo huo zitatandazwa Februari 16, 2023 kabla ya marudiano kufanyika wiki moja baadaye. Man-United watatangulia kutua ugani Camp Nou kabla ya kualika Barcelona uwanjani Old Trafford.

Chini ya kocha Erik ten Hag, Man-United waliambulia nafasi ya pili nyuma ya Real Sociedad katika Kundi E la Europa League huku Barcelona wakiridhika na nafasi ya tatu nyuma ya Inter Milan na Bayern Munich katika Kundi C la UEFA.

Jose Mourinho ataongoza waajiri wake AS Roma kuchuana na FC Salzburg huku Sporting Lisbon wakimenyana na Midtjylland. Shakhtar Donetsk watakwaruzana na Rennes, Ajax waonane na Union Berlin nao Leverkusen wapambane na AS Monaco. Sevilla watakabiliana na PSV Eindhoven.

DROO YA MCHUJO WA EUROPA LEAGUE:

Barcelona vs Man-United

Juventus vs Nantes

Sporting vs Midtjylland

Shakhtar Donetsk vs Rennes

Ajax vs Union Berlin

Leverkusen vs Monaco

Sevilla vs PSV Eindhoven

FC Salzburg vs Roma

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Mrembo mwenye azma ya kuvuna sifa kama Lionel Messi

Liverpool wapewa tena Real Madrid huku Bayern Munich...

T L