• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Napoli wapepeta wanyonge Cremonese na kufungua pengo la pointi 16 kileleni mwa jedwali la Serie A

Napoli wapepeta wanyonge Cremonese na kufungua pengo la pointi 16 kileleni mwa jedwali la Serie A

Na MASHIRIKA

NAPOLI waliweka hai matumaini ya kutawazwa wafalme wa Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mara ya kwanza tangu 1989-90 baada ya kukomoa wanyonge Cremonese 3-0 mnamo Jumapili na kufungua mwanya wa alama 16 kati yao na nambari mbili Inter Milan kileleni mwa jedwali.

Mabao kutoka kwa Khvicha Kvaratskhelia, Victor Osimhen na Eljif Elmas yaliwapa Napoli ushindi wao wa 19 ligini baada ya mechi 22 za msimu huu.

Napoli sasa wameshinda mechi sita mfululizo na wamepoteza alama saba pekee ligini msimu huu wa 2022-23. Hata hivyo, pengo la alama kati yao na Inter Milan litapunguzwa kwa pointi tatu zaidi iwapo Inter watacharaza Sampdoria mnamo Februari 13, 2022.

Katika mechi nyingine ya Serie A mnamo Jumapili, Juventus walisajili ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Fiorentina. Bao la pekee na la ushindi katika pambano hilo lilijazwa kimiani na Adrien Rabiot.

Matokeo hayo yalishuhudia Juventus waliopokonywa alama 15 mnamo Januari kwa hatia kwenye soko la uhamisho wa wachezaji wakipaa hadi nafasi ya tisa jedwalini kwa pointi 29 sawa na Monza na Bologna.

MATOKEO YA SERIE A (Jumapili):

Napoli 3-0 Cremonese

Udinese 2-2 Sassuolo

Bologna 0-1 Monza

Juventus 1-0 Fiorentina

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Washukiwa 8 washtakiwa kwa wizi wa mikopo ya Fuliza

Southampton wamtimua kocha Nathan Jones

T L