• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Olunga kuonyesha waajiri wake wa Al Duhail kuwa anaweza

Olunga kuonyesha waajiri wake wa Al Duhail kuwa anaweza

Na GEOFFREY ANENE

NYOTA Michael Olunga amesema mashindano ya Klabu Bingwa Asia yatampa fursa ya kuthibitisha kuwa yeye ni mshambuliaji anayeweza kutegemewa na waajiri wake wapya, Al Duhail.

Katika kikao na wanahabari uwanjani King Abdullah mjini Jeddah, ambako mechi za Kundi C dhidi ya Al Shorta (Iraq), Al Ahli Saudi (Saudi Arabia) na Esteghlal (Iran), Mkenya huyo alisema kuwa atajituma vilivyo kusaidia timu yake kutinga raundi ya pili.

Olunga, ambaye alisherehekea kufikisha umri wake miaka 27 mnamo Machi 26, aliongeza, “Kundi letu, jinsi kocha alisema, ni ngumu ambalo linajumuisha klabu nzuri na kila klabu iko hapa kutafuta ushindi ili iingie raundi ya pili. Tutatafuta matokeo mazuri kwa kuonyesha uwezo na nguvu ambazo Al Duhail inazo za kuingia raundi ijayo. Hata hivyo, lazima tumakinike uwanjani.”

Al Duhail ya kocha Sabri Lamouchi itaanza kampeni yake dhidi ya maafisa wa polisi kutoka Iraq, Al Shorta mnamo Aprili 15 saa tatu kasorobo usiku.

Olunga amefungia Al Duhail mabao 10 katika michuano 15 iliyopita tangu awasili kutoka Kashiwa Reysol nchini Japan mnamo Januari 12. Aliibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Japan mwaka 2020 baada ya kucheka na nyavu mara 28. Mechi za Kundi C zimeratibiwa kusakatwa Aprili 15 hadi Aprili 30.

  • Tags

You can share this post!

KCB yajiondoa kwenye mashindano ya Bara Afrika ya voliboli...

Wanaraga wa Kenya wanaocheza ughaibuni wafika 10