Na MASHIRIKA
REAL Madrid walisajili ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Real Betis katika mechi ya Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumamosi usiku.
Miamba hao wanaoendelea kuwania huduma za fowadi matata wa Paris Saint-Germain (PSG), Kylian Mbappe kwa Sh21.4 bilioni, walifungiwa bao la pekee na la ushindi na beki Dani Carvajal aliyekamilisha krosi ya Karim Benzema katika dakika ya 61.
Betis walipoteza nafasi nyingi za kusawazisha kupitia kwa mvamizi raia wa Ufaransa, Nabil Fekir.
Ushindi wa Real uliwakweza kileleni mwa jedwali la La Liga baada ya michuano mitatu ambayo imevunia alama saba sawa na Sevilla, Valencia na Mallorca.
Kufikia sasa, Real ambao wamekadiria hasara ya Sh33 bilioni tangu watikiswe na janga la corona mnamo Januari 2020, wamesajili mchezaji mmoja pekee – beki David Alaba aliyeagana na Bayern Munich ya Ujerumani bila ada yoyote mwishoni mwa msimu wa 2020-21.
MATOKEO YA LA LIGA (Agosti 28, 2021):
Real Betis 0-1 Real Madrid
Celta Vigo 0-1 Bilbao
Elche 1-1 Sevilla
Sociedad 1-0 Levante
TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO