• Nairobi
  • Last Updated May 10th, 2024 5:15 PM
Real Madrid wapiga Betis na kutua kileleni mwa jedwali la La Liga

Real Madrid wapiga Betis na kutua kileleni mwa jedwali la La Liga

Na MASHIRIKA

REAL Madrid walisajili ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Real Betis katika mechi ya Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) mnamo Jumamosi usiku.

Miamba hao wanaoendelea kuwania huduma za fowadi matata wa Paris Saint-Germain (PSG), Kylian Mbappe kwa Sh21.4 bilioni, walifungiwa bao la pekee na la ushindi na beki Dani Carvajal aliyekamilisha krosi ya Karim Benzema katika dakika ya 61.

Betis walipoteza nafasi nyingi za kusawazisha kupitia kwa mvamizi raia wa Ufaransa, Nabil Fekir.

Ushindi wa Real uliwakweza kileleni mwa jedwali la La Liga baada ya michuano mitatu ambayo imevunia alama saba sawa na Sevilla, Valencia na Mallorca.

Kufikia sasa, Real ambao wamekadiria hasara ya Sh33 bilioni tangu watikiswe na janga la corona mnamo Januari 2020, wamesajili mchezaji mmoja pekee – beki David Alaba aliyeagana na Bayern Munich ya Ujerumani bila ada yoyote mwishoni mwa msimu wa 2020-21.

MATOKEO YA LA LIGA (Agosti 28, 2021):

Real Betis 0-1 Real Madrid

Celta Vigo 0-1 Bilbao

Elche 1-1 Sevilla

Sociedad 1-0 Levante

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

You can share this post!

Matasi aahidi kusaidia Tusker FC kuzoa mataji baada ya...

Lewandowski afungia Bayern Munich mabao matatu na kuvunja...