• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 7:55 PM
Rekodi ya Kamworor yafutwa Antrim Half Marathon

Rekodi ya Kamworor yafutwa Antrim Half Marathon

Na GEOFFREY ANENE

REKODI za Uingereza za mbio za kilomita 21 za Wakenya Geoffrey Kamworor na Edith Chelimo zimefutwa na Jemal Yimer na Yalemzerf Yehualaw nchini Northern Ireland baada ya Waethiopia hao kushinda Antrim Coast Half Marathon, Jumapili.

Jimer ametwaa taji la wanaume kwa dakika 59:04 akivunja rekodi ya 59:10 ambayo Kamworor aliweka mjini Cardiff mwaka 2016. Alikamilisha dakika moja na sekunde 56 mbele ya nambari mbili Alfred Ng’eno kutoka Kenya (saa 1:01:00) naye Shadrack Kimining pia kutoka Kenya akafunga tatu-bora (1:01:08).

Yehualaw alinyakua taji la kinadada kwa saa 1:04:22, muda ambao ni sekunde 91 bora kuliko ule wa Chelimo. Alifuatiwa kwa karibu na Muethiopia mwenzake Tsehay Gemechu (1:05:01) naye Mkenya Beatrice Chepkemoi akakamilisha nafasi tatu za kwanza kwa 1:07:37).

Mashindano haya ya kila mwaka yalivutia mamia ya washiriki wakiwemo 79 katika kitengo cha mbio za kilomita 21. Washikilizi wa tatu za kwanza walizawadiwa Sh602,519, Sh301,259 na Sh241,007 mtawalia. 

  • Tags

You can share this post!

Mkasa wa moto wasababisha kifo cha mtu mmoja, familia...

Arsenal wakanyaga Fulham na kuendeleza ubabe wao katika EPL...

T L