• Nairobi
  • Last Updated May 6th, 2024 2:59 PM
Sasa Man-United yakanusha madai kumhusu Ronaldo

Sasa Man-United yakanusha madai kumhusu Ronaldo

MANCHESTER, Uingereza

Na MASHIRIKA

KLABU ya Manchester United imekanusha madai kwamba inapanga kumpa Cristiano Ronaldo jukumu la kuwa kocha mkuu atakapostaafu.

Kumekuwa na uvumi kwamba klabu hiyo inawazia kumuajiri mshambulijai huyo mwenye umri wa miaka 36, mara tu akiangika daluga zake.

Ronaldo alijiunga tena na United kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Juventus ambao walimng’oa Real Madrid, alikoenda 2009 akitokea Old Trafford.

Tayari mwanawe Cristiano Junior amesajiliwa katika akademia ya United, hali inayofanya mashabiki kusambaza uvumi huo.Wengine wanadai Ronaldo ndiye atamrithi Ole Gunnar Solskjaer ili aweze pia kufuatilia ukuaji wa kisoka wa mwanawe huyo mwenye umri wa miaka 11.

You can share this post!

Washukiwa wa wizi wa mabomba ya maji wanaswa

Muujiza wa Conte kutoa maji kwenye mwamba pale Spurs

T L