• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 7:50 AM
Timu 10 kushiri Mini-ligi ya Kaunti ya Taita Taveta wikendi

Timu 10 kushiri Mini-ligi ya Kaunti ya Taita Taveta wikendi

NA ABDULRAHMAN SHERIFF

KLABU sita za wanaume na nyingine nne za wanawake zilizoshiriki ligi za kaunti ndogo na kumaliza nafasi za juu zinatarajia kupambana mjini Mwatate leo na kesho Jumapili kupigania taji la Klabu Bingwa wa Kaunti ya Taita Taveta.

Katibu wa Shirikisho la Kandanda la nchini (FKF) tawi la Taita Taveta, Basil Mwakulomba amesema mechi hizo zitaanza rasmi saa tatu za asubuhi na zinatarajia kufikia fainali hapo kesho kuanzia saa nane mchana.Timu za wanaume zitakazoshiriki ni Kingstone FC ya Voi, Kamtonga FC ya Mwatate na Kimala FC ya Taveta ambazo ziko katika Kanda A hali Kanda B itakuwa na Tsunami ya Voi, Rising Stars ya Mwatate na Eldoro Sports Villa FC ya Taveta.

Mechi ya kwanza ya Kanda A itakuwa baina ya Kingstone na Kamtunga itakayochezwa uwanja wa Mwatunge saa tatu asubuhi hali mchezo wa kwanza wa Kanda B utakuwa kati ya Eldoro Sports Villa na Rising Stars ambao utafanyika uwanja wa Ziwa saa tatu asubuhi.

Mechi nyingine zitachezwa kama ifuatavo: Kanda A saa sita mchana: Kamtong na Kimala na saa tisa alasiri: Kimala na Kingstone. Kanda B- Saa sita mchana: Rising Stars na Tsunami na saa tisa alasiri: Tsunami vs Eldoro Sports Villa. Kwa upande wa soka la wanawake, Mwakulomba amesema timu nne zitakazoshiriki ni nne ambazo ni Weavers Birds FC ya Voi, Simba Ladies FC ya Wundanyi, Pema Ladies FC ya Mwatate na Gichea Queens FC ya Taveta.

“Timu nne hizi za wanawake zitapiga kura ipi itakutana na ipi na mechi zake za nusu fainali moja itachezwa uwanja wa Mwandisha na nyingine uwanja wa Sisal siku ya Jumapili saa tatu asubuhi na fainali kufanyika uwanja wa Mwandisha hapo saa nane,” akasema katibu huyo.

You can share this post!

Tusker, Gor zalenga ushindi Caf kesho

Mwendwa anaswa tena

T L