• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 6:30 PM
Vihiga Queens, Nakuru City Queens kitaeleweka ligini KWPL leo Jumamosi

Vihiga Queens, Nakuru City Queens kitaeleweka ligini KWPL leo Jumamosi

NA AREGE RUTH

KIVUMBI kikali kinatarajiwa wikendi hii kati ya vinara wa ligi Vihiga Queens na Nakuru City Queens ugani Mumias Complex katika raundi ya 10 ya mechi ya Ligi Kuu ya Wanawake nchini (KWPL).

Timu hizi zimeachana kwa alama mbili kwenye jedwali. Vihiga wanashikilia nafasi ya kwanza na alama 19 nao Nakuru wanafunga nne bora na alama 17.

Katika shule ya upili ya Dagoretti High jijini Nairobi, Kangemi Ladies watakuwa wanatafuta alama muhimu ambazo zitawatoa mkiani kwenye jedwali, watakapo menyana na wa wanajeshi wa Ulinzi Starlets leo Jumamosi.

Kwingineko, mabingwa watetezi Thika Queens wanapanga kuwavamia Kayole Starlets katika uwanja wa Manisapaa ya Thika kaunti ya Kiambu.

Wakati huo huo, Gaspo Women watamenyana na Wadadia Women ugani GEMS Cambridge kaunti ya Kajiado.

Bunyore Starlets nao watawaalika Trans Nzoia Falcons kichinjioni uwanjani Mumboha kaunti ya Vihiga. Kisumu All Starlets watafunga shughuli ya siku dhidi ya Zetech Sparks ugani Moi mjini Kisumu.

Mechi sita zitachezwa wikendi hii kuanzia leo Jumamosi hadi kesho Jumapili. Huku mechi za mkondo wa kwanza zikielekea kukamilika, ligi itachukua mapumziko mafupi baadaye wikendi ijayo.

  • Tags

You can share this post!

Tahadhari uchaguzi Nigeria ukianza leo Jumamosi

Madai ya unyanyasaji wa kingono Kericho yachunguzwa na...

T L