• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 7:15 PM
Vipusa wa Man-City wakomoa Fiorentina 8-0 na kufuzu kwa robo-fainali za UEFA

Vipusa wa Man-City wakomoa Fiorentina 8-0 na kufuzu kwa robo-fainali za UEFA

Na MASHIRIKA

MANCHESTER City walipepeta Fiorentina 5-0 mnamo Alhamisi ya Machi 11, 2021 jijini Florence, Italia na kufuzu kwa robo-fainali za Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) kwa Wanawake.

Man-City waliwekwa kifua mbele na Ellen White aliyefunga mabao mawili kabla ya Caroline Wier kuzamisha kabisa chombo cha wenyeji wao kunako dakika ya 70. Sam Mewis pia alipachika wavuni magoli mawili katika kipindi cha pili kwenye gozi hilo la hatua ya 16-bora.

Ushindi huo mnono uliosajiliwa na Man-City uliwasaidia kuwabandua Fiorentina ya Italia kwa jumla ya mabao 8-0.

Matokeo hayo yanamaanisha kwamba Man-City sasa wana uhakika wa kusonga mbele zaidi katika kipute cha UEFA kuliko jinsi walivyofanya katika muhula wa 2019-20 ambapo waliondolewa na Atletico Madrid ya Uhispania kwenye hatua ya 16-bora.

Atletico walidenguliwa na Chelsea ambao ni mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake nchini Uingereza (WSL) katika hatua ya 16-bora ya UEFA msimu huu kwa jumla ya mabao 3-1. Hii ni baada ya kikosi hicho kulazimishiwa sare ya 1-1 katika mchuano wa mkondo wa pili uliochezewa nchini Uhispania mnamo Machi 10, 2021.

Man-City walijitosa ugani kuvaana na Fiorentina kwenye marudiano ya Alhamisi wakijivunia motisha ya kuwapepeta Everton katika ushindi wao wa tisa mfululizo kwenye kipute cha WSL.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Man-United padogo kuaga Europa League baada ya AC Milan...

Rangers na Slavia nguvu sawa katika mkondo wa kwanza Europa...