• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 7:05 PM
VITUKO: Sasa mrembo Ivana awinda penzi la Jesus huku kipusa Elle akimtaka Haaland

VITUKO: Sasa mrembo Ivana awinda penzi la Jesus huku kipusa Elle akimtaka Haaland

IMEKUSANYWA NA CHRIS ADUNGO

MWANAMITINDO maarufu mzawa wa Ujerumani na raia wa Croatia, Ivana Knoll, sasa asema tamanio lake ni kumfungulia sogora Gabriel Jesus wa Arsenal buyu lake la asali.

“Napenda Arsenal na ninamtamani Gabriel (Jesus). Nitampa ufunguo wa mzinga mzima akipona na kurejea ugani kutuongoza kushinda ligi msimu huu,” akaandika kwenye Instagram.

Mrembo huyo alionekana baadaye akiponda raha katika mkahawa wa kifahari wa Cirque Le Soir ulioko Soho, London, Uingereza.

Mwezi mmoja umekatika tangu Jesus, 25, abwagane na mchumba wake, Raiane Lima; hiyo ikiwa miezi minane baada ya uhusiano wao kujaliwa mtoto wa kike, Helena.
Mvamizi huyo wa zamani wa Manchester City amewahi pia kula bata na kidege Ludimilla Oliveira.

Ivana atakumbukwa kwa kuzengua mashabiki wakati wa Kombe la Dunia nchini Qatar mwezi Desemba.

Licha ya masharti makali yanayodhibiti mavazi ya wanawake Qatar, Ivana alinyegeresha wengi katika mechi za Croatia kwa kuvalia nguo fupi zilizoacha nje sehemu kubwa ya mwili wake.

Kwingineko, kisura Elle Brooke amefunguka na kukiri kwamba anatamani sana tunda lake lidokolewe na fowadi matata wa Manchester City, Erling Haaland.

Elle ambaye ni bondia na mwanamitindo maarufu nchini Uingereza, analianika penzi lake kwa Haaland miezi mitatu baada ya sogora huyo wa Man-City kufichua kuwa anakula bata na kipusa Isabel Haugseng Johansen, ambaye pia mwanasoka kutoka Norway.

Umaarufu ulianza kumuandama mwanamitindo huyo mzawa wa Ujerumani mnamo 2014 nchini Brazil alipohudhuria mechi nyingi akiwa nusu-uchi.

Aliwahi kujitosa ugani tuputupu makala ya 2018 nchini Urusi baada ya Croatia kudengua Uingereza 2-1 katika nusu-fainali.

Kwingineko, kisura Elle Brooke amefunguka na kukiri kwamba anatamani sana tunda lake lidokolewe na fowadi matata wa Manchester City, Erling Haaland.

Elle ambaye ni bondia na mwanamitindo maarufu nchini Uingereza, analianika penzi lake kwa Haaland miezi mitatu baada ya sogora huyo kufichua kuwa anakula bata na kipusa Isabel Haugseng Johansen ambaye pia ni mwanasoka kutoka Norway.
Ili kumtia Haaland kishawishini wiki hii, Elle alipakia mitandaoni baadhi ya picha alizopigwa akiwa ameacha wazi sehemu kubwa ya mwili wake.

Chini ya mojawapo ya picha aliandika: “Nikague rafiki. Umeona kinachokupendeza? Vyote kwa ajili yako, wakati wowote. Basi nitakuwa uwanjani kuhudhuria kila mechi utakayopiga.”

Mnamo Novemba 2022. Haaland na Isabel walionekana hadharani kwa mara ya kwanza wakiponda raha katika ufuo wa Marbella nchini Uhispania.

Haaland alitumia baadaye mahojiano yake na gazeti la The Sun kufichua jinsi anavyowaniwa kimapenzi na idadi kubwa ya warembo tangu umaarufu uanze kumwandama katika ulingo wa soka akichezea RB Salzburg ya Austria na Borussia Dortmund ya Ujerumani.

  • Tags

You can share this post!

NYOTA WA WIKI: Alejandro Garnacho

Arsenal wasubiri hadi dakika za mwisho kuzamisha chombo cha...

T L