• Nairobi
  • Last Updated May 7th, 2024 9:48 PM
Page kuendelea kutekeleza majukumu ya kocha Ryan Giggs katika timu ya taifa ya Wales

Page kuendelea kutekeleza majukumu ya kocha Ryan Giggs katika timu ya taifa ya Wales

Na MASHIRIKA

KOCHA msaidizi wa Wales, Robert Page, ataendelea kutekeleza majukumu ya mkufunzi mkuu wa timu hiyo, Ryan Giggs, katika mechi tatu zijazo za kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia zitakazoandaliwa nchini Qatar mnamo 2022.

Mnamo Novemba, Giggs alitiwa nguvuni kwa tuhuma za kumjeruhi mpenzi wake aliyezozana naye wakiwa nyumbani. Muda wa dhamana aliyopewa kutokana na hatia hiyo ulirefusha hadi Mei 2021.

Wales wamepangwa kuanza kampeni zao za kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Ubelgiji mnamo Machi 24 ugenini kabla ya kualika Mexico kwa mechi ya kirafiki mnamo Machi 27. Baada ya hapo, wameratibiwa kucheza na Jamhuri ya Czech jijini Cardiff kwenye mchuano mwingine wa kufuzu kwa Kombe la Dunia mnamo Machi 30.

Shirikisho la Soka la Wales (FAW) limeafikiana na Giggs kuhusu jinsi majukumu yake yatakavyoendeshwa na Page katika maandalizi ya kikosi kwa minajili ya kampeni zijazo za kufuzu kwa Kombe la Dunia.

Kwa mujibu wa FAW, Page atasaidiwa sasa na Albert Stuivenberg aliyempiga jeki wakati wa mechi nyinginezo za kimataifa zilizosakatwa na Wales mnamo Novemba 2020.

Page ambaye atakuwa akishauriana pakubwa na Giggs kupitia simu na barua-pepe, alisimamia michuano mitatu iliyopita ya Wales dhidi ya Amerika, Jamhuri ya Ireland na Finland.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Manchester City roho juu ikiwaalika Southampton leo...

Korti yaelezwa Lali alikuwa na mazoea ya kumgombeza mpenzi...