• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Helikopta yaibua msisimko katika kampeni za Muthama

Helikopta yaibua msisimko katika kampeni za Muthama

NA STEPHEN MUTHINI

MWENYEKITI wa UDA na mwaniaji wa kiti cha Ugavana wa Machakos Johnstone Muthama, amekuwa akidhihirisha ukwasi wake kwa kuendesha kampeni kali akitumia helikopta katika kaunti hiyo.

Mnamo Jumatatu, Bw Muthama ambaye ni bwanyenye aliandaa mikutano minane katika maeneobunge ya Masinga na Yatta kabla ya kufanya mingine sita kaunti ndogo za Mwala, Kangundo na Mavoko mnamo Jumatano.

Matumizi ya helikopta yamekuwa yakivutia umati katika mikutano yake huku wanakijiji wengi, hasa mashinani wakifurahia kutazama ndege hiyo kwa karibu.

Katika mikutano hiyo, aliandamana na mgombeaji mwenza Faith Muli na wawaniaji wa UDA kwenye nyadhifa za Useneta na Mwakilishi wa Kike wakili Joel Kyatha Mbaluka na Anna Ndilo.

“Nipeni kura za ugavana na utamwona waziri wa ardhi hapa akiwakabidhi vyeti vya ardhi. Na iwapo hilo halitatekelezwa, hamtaniona tena mbele yenu,” akasema Bw Muthama alipokuwa akihutubia maelfu ya wafuasi wake katika eneo la Ndithini, eneobunge la Masinga.

Kampeni za Bw Muthama yamkini zimeimarika zaidi hivi karibuni baada ya kutoweka awali na kuibua maswali iwapo alikuwa kwenye kiny’ang’anyiro cha ugavana.

“Nimekuja hapa kuwahakikishia ninawania ugavana,” akasema.

You can share this post!

Shahbal avunja nyoyo za wafuasi kwa kujiondoa uchaguzini

Raila apokonywa mamlaka ya kuteua mgombeaji mwenza wake

T L