• Nairobi
  • Last Updated May 12th, 2024 7:50 AM
Kabando adai ubaguzi ndani ya Azimio Nyeri

Kabando adai ubaguzi ndani ya Azimio Nyeri

NA JAMES MURIMI

MWANIAJI wa useneta Kaunti ya Nyeri kupitia Narc Kenya, Kabando Wa Kabando amelalamika kuwa timu inayoendesha kampeni ya muungano wa Azimio Kaunti hiyo ina ubaguzi.

Alilalamika kuwa kuna watu wanaopiga vita azma yake ya kuwania kiti hicho.

“Timu inayoongoza kampeni ya Azimio Nyeri inanipiga vita. Watu hao hawaelewi kuwa ni wananchi ndio watakaofanya uamuzi. Walivuruga kampeni ya kiongozi wa chama chetu, Martha Karua na wanalenga kuzima azma yangu,” Bw Kabando akaandika kwenye mtandao wake wa Twitter.

Kinara wa ODM, Raila Odinga na mgombea mwenza wake Jumanne, walijipigia debe katika maeneo ya Chaka, Karatina, Mukurwe-ini, Othaya, Giakanja na Nyeri.

Bw Kabando na aliyekuwa mwakilishi wa jinsia ya kike Nyeri, Priscilla Nyokabi (Jubilee) walitoa wito Kwa Bw Odinga na mwaniaji mwenza wake kusuluhisha suala la njaa, karo na kuimarisha sekta ya afya.

“Karibuni Nyeri Bi Karua na Bw Odinga. Tunaomba sekta ya elimu na afya ziimarishwe,” akasema Bw Kabando.

  • Tags

You can share this post!

Kibarua ashtakiwa kwa kuvunja vioo vya madirisha ya kituo...

Wiper iliteua Sonko naibu wa Mbogo – wakili aeleza

T L