• Nairobi
  • Last Updated May 21st, 2024 8:55 PM
Kindiki ahimizwa akubali uwaziri Ruto akishinda urais Agosti

Kindiki ahimizwa akubali uwaziri Ruto akishinda urais Agosti

NA ALEX NJERU

SENETA wa kaunti ya Tharaka Nithi Profesa Kithure Kindiki, amehimizwa kukubali wadhifa wa waziri mwenye nguvu iwapo Naibu Rais William Ruto, atashinda urais kwenye uchaguzi mkuu wa Agosti 9.

Akizungumza katika hafla ya kuzindua mwaniaji mwenza wa Gavana wa Tharaka Nithi Muthomi Njuki katika uwanja wa Kairuni , Jumapili, mbunge wa Maara, Bw Kareke Mbiuki, alisema baada ya kukosa kuteuliwa mwaniaji mwenza wa Dkt Ruto, Prof Kindiki anafaa kuchagua wizara anayotaka kusimamia.

Alimhimiza Prof Kindiki kutokubali wadhifa wa Mwanasheria Mkuu, kwa kuwa hautawasaidia watu wake ambao wangenufaika pakubwa kama angekuwa naibu rais.

“Tunataka Kindiki kuchagua Wizara ya Uchukuzi kwa sababu changamoto yetu kubwa ni barabara mbaya,” alisema mbunge huyo.

Alisema ingawa Kindiki hakuteuliwa mwaniaji mwenza wa Dkt Ruto, huenda kaunti ya Tharaka Nithi ikapata waziri wa kwanza iwapo Ruto atashinda urais kwenye uchaguzi wa Agosti 9.

Mbunge wa Chuka/Igambang’ombe Bw Patrick Munene alihimiza eneo la Mlima Kenya kutoshawishiwa kupigia kura mwaniaji urais wa muungano wa Azimio la Umoja One Kenya Raila Odinga kwa sababu ya kumteua kiongozi wa Narc Kenya Martha Karua kuwa mwaniaji mwenza wake.

  • Tags

You can share this post!

Kanisa lajitenga na mwanamume anayedaiwa kuwachoma wavulana...

TANZIA: Mbunge William Kamoti afariki baada ya gari lake...

T L