• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 10:50 AM
Maangi asema atahepa Ruto Matiang’i akiwania

Maangi asema atahepa Ruto Matiang’i akiwania

Na Wycliffe Nyaberi

NAIBU Rais William Ruto huenda akakosa uungwaji mkono katika eneo la Gusii iwapo Waziri wa Usalama Dkt Fred Matiang’i atawania Urais 2022.

Naibu Gavana wa Kisii Joash Maangi ambaye ni mwandani wa Dkt Ruto, jana alisema kuwa atamuunga mkono Dkt Matiang’i akiwania.

Bw Maangi, ambaye amekuwa akiendesha shughuli zote za chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika eneo la Gusii, alisema hayo siku mbili baada yake na wanasiasa wengine wa Tangatanga kutoka kaunti za Nyamira na Kisii, kukutana na Dkt Ruto jijini Nairobi, Alhamisi.

“Unajua mimi nalenga kuwa gavana wa Kisii na iwapo ‘mtoto’ wetu Matiang’i atawania urais, bila shaka jamii yote itakuwa nyuma yake na haitamsikiza mtu yeyote atakayekwenda kinyume. Nitaonekana mtu mjinga kumpinga kwani huo utakuwa mwisho wangu kisiasa na nitatumwa kijijini mapema asubuhi,” akasema Bw Maangi.

 

You can share this post!

Wazee wa Kaya sasa wavuruga karata za Jumwa

Argentina wakung’uta Brazil na kutwaa taji la Copa...