• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 8:50 AM
ODM yafifia Jubilee ikivuna ngome zake

ODM yafifia Jubilee ikivuna ngome zake

Na BERNARDINE MUTANU

CHAMA cha ODM kimepoteza umaarufu kwa Jubilee katika ngome zake za Pwani, Nyanza na Magharibi.

Kwa sasa, Jubilee ndicho chama maarufu zaidi kulingana na ripoti ya utafiti uliofanywa na kampuni ya utafiti ya Infotrak.

Ripoti hiyo iliyotolewa jana, ilionyesha kuwa Wakenya wengi zaidi (asilimia 40) wanajihusisha na chama cha Jubilee dhidi ya asilimia 21 wanaojihusisha na ODM.

Ni asilimia tatu pekee ya wote waliohusishwa katika utafiti huo waliounga mkono na chama cha Wiper Democratic-Movement Kenya (WDM-K).

Nayo asilimia moja pekee inaunga mkono Amani National Congress (ANC) na pia FORD-Kenya.

Cha kushangaza ni kuwa, licha ya Jubilee kuendelea kupata umaarufu katika ngome za ODM, chama cha Chungwa kimepoteza ufuasi katika maeneo kinakotarajiwa kuwa na wafuasi wengi zaidi.

Kwa mfano, katika eneo la Nyanza, ni asilimia 47 waliosema ni wafuasi wa ODM dhidi ya asilimia 24 waliounga mkono Jubilee.

Kwa upande mwingine, umaarufu wa Jubilee eneo la Kati umesalia imara kwa asilimia 61, dhidi ya umaarufu wa ODM wa asilimia saba pekee.

Katika eneo la Pwani, vyama hivyo maarufu zaidi nchini vina uwezo sawa, ambapo asilimia 33 ya wakazi wa eneo hilo (kwa kila chama) walisema wanaviunga mkono.

Na katika eneo la Magharibi, umaarufu wa ODM umedidimia dhidi ya umaarufu wa Jubilee ambapo ni asilimia 25 pekee wanaounga mkono chama hicho kinachoongozwa na Raila Odinga dhidi ya asilimia 27 wanaounga mkono Jubilee.

Hali ni kama hiyo katika Kaunti ya Nairobi ambapo ODM kina umaarufu wa asilimia 27 dhidi ya asilimia 23 ya Jubilee.

Chama cha Jubilee kina wafuasi wengi zaidi eneo la Bonde la Ufa kwa asilimia 57 dhidi ya asilimia 12 wanaounga mkono chama cha ODM.

Licha ya mgogoro wa ndani ambao umetishia kusambaratisha Jubilee, bado chama hicho ni maarufu zaidi eneo la Kaskazini Mashariki (asilimia 42) na Mashariki (asilimia 39).

You can share this post!

Viongozi wataka Uhuru atatue shida za Jubilee

JSC kuamua majaji 11 wanaofaa kwa Mahakama ya Rufaa

adminleo