NA CHARLES WASONGA
RAIS Uhuru Kenyatta amekariri kujitolea kwake kusimamia mpito wa mamlaka kwa njia ya amani kwa utawala ujao wa Rais mteule William Ruto.
Kwenye hotuba yake kwa taifa Jumatatu jioni, Rais Kenyatta hata hivyo alionekana kutilia shaka uamuzi wa Mahakama ya Upeo ambao uliidhinisha ushindi wa Dkt Ruto.
“Nitatekeleza maagizo ya mahakama hii kikamilifu,” akasema.
“Nitahakikisha kuwa mpito wa utawala hadi utawala ujao umefanyika kikamilifu na maagizo ya kufanikisha mchakato huo tayari yametolewa,” Rais Kenyatta akasema.
Lakini akaongeza hivi: “Ni jambo la kushangaza kuwa asasi hiyo imetoa uamuzi ambao hauakisi hali halisi kuhusu kuhusu matukio katika zoezi lililofanyika Agosti.”
Aidha, Rais Kenyatta hakumtaja Dkt Ruto kwa jina, ila alichukua fursa hiyo kuwapongeza wagombeaji wote walioshiriki katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9.