NA KNA
TUME Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), imewaidhinisha wagombeaji wote 13 wa ugavana waliotathminiwa Kaunti ya Taita Taveta.
Ushindani mkali sasa unatarajiwa kwa uwaniaji wa kiti hicho kinachoshikiliwa na Gavana Granton Samboja (pichani), atakayejitetea kupitia Chama cha Jubilee baada ya kuhama Wiper.
Msimamizi mkuu wa uchaguzi kaunti hiyo, Bi Eisha Mohamed, alisema shughuli nzima ya kutathmini wagombeaji ilifanywa bila matatizo. Aliongeza kuwa jukumu sasa ni la wanasiasa kudumisha amani wakati wote wa kampeni.