NA JANET KAVUNGA
KILIFI MJINI
KIZAAZAA kilizuka katika hoteli moja mjini hapa jamaa na demu wake waliporushiana cheche kali za matusi.
Wawili hao walifika hotelini wakionekana kuwa na furaha na wakaketi katika meza moja kufurahia mlo na vinywaji huku wakipiga gumzo.
Baada ya muda, demu alilipuka kwa hasira naye jamaa akachemka vile vile.
“Ulifuatia ugomvi mkali kila mmoja wao akirushia mwenzake maneno yasiyoweza kuchapishwa,” alisema mdokezi.
Walianikana mbele ya wateja ambao walisitisha starehe zao kutazama sinema ya bure.
Jamaa alipotisha kumtwanga demu, walinzi wa hoteli hiyo waliitwa na kuwasukuma kwa keshia walipe bili zao kabla ya kufurushwa nje.
Mdokezi asema kila mmoja alipanda gari lake na kuondoka kwenda zake ndipo wateja wakarudia starehe zao baada ya mapumziko mafupi yaliyosababishwa na wawili hao.