• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 11:13 AM
Afanyiwa kiini macho akapapasa nyani akidhani ni kimada wake

Afanyiwa kiini macho akapapasa nyani akidhani ni kimada wake

NA JANET KAVUNGA

SOKOKE, KILIFI

JAMAA aliyekuwa akinyemelea mke wa mtu alijipata pabaya alipofanyiwa kiini macho na mume wa mwanadada huyo, akabaki kukumbatia nyani kwenye kichaka alichokuwa akisubiri windo lake ili wajipe raha.

Jombi alikuwa ameonywa na mume wa mwanadada akome kuchovya asali yake, lakini kiburi na dharau zilimfanya apuuze onyo hilo.

Siku ya kioja, alipanga na mwanadada wakutane katika kichaka kimoja na akawahi mapema kumsubiri.

Akiwa hapo, aliona demu amefika na akamkumbatia kwa furaha.

Lakini alipojaribu kumpiga busu aligutuka kugundua amepakata nyani.

Polo alipiga nduru akachomoka haraka kutoka kichakani huku akifyatuka mbio kama mwizi.

Mtu wa kwanza kuitikia nduru zake alikuwa ni mume wa mwanadada ambaye alikuwa akinyemelea.

Jombi aliongeza kasi ya mbio pasipo kuangalia nyuma. Tangu siku hiyo akaacha kutamani wake wa watu.

  • Tags

You can share this post!

Msimu mpya wa mbio za nyika kuanza Oktoba 14 mjini Machakos

Visa vya moto, migomo vyaongezeka katika shule za Ganze...

T L