• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 10:44 AM
Jombi ashindwa kula siku tatu baada ya kugundua aliyepanga kuoa ni mke wa mtu

Jombi ashindwa kula siku tatu baada ya kugundua aliyepanga kuoa ni mke wa mtu

Na JANET KAVUNGA

LIKONI, MOMBASA

JOMBI mmoja wa hapa alivunjika moyo hadi akashindwa kula kwa siku tatu baada ya kugundua kwamba mwanadada aliyepanga kuoa alikuwa mke wa mtu.

Jamaa alikutana na demu katika hoteli wanakofanya kazi na wakaanza uhusiano wa kimapenzi kwa kuwa mwanadada alimweleza hakuwa ameolewa.

Alimwambia jamaa alikuwa akisaka mpenzi watakayefunga pingu za maisha na jombi akaamini alikuwa amepata mwanadada chaguo la mke.

Juzi, demu alikosa kufika kazini na jioni ya siku hiyo, jamaa akamtembelea kujua kilichompata.

Jombi hakuamini alipopata demu akiwa ametembelewa na mumewe na mtoto wao wanaoishi ushago.

“Alirudi kwake akiwa amevunjika moyo hadi akashindwa kula kwa siku tatu. Ni bahati tu hakutwangwa na mume wa mwanadada huyo,” alieleza mdokezi.

  • Tags

You can share this post!

Subirini kidogo tu, hali itakuwa shwari, Ruto ahakikishia...

Serikali kuchunguza kiwango cha fedha inachopoteza kila...

T L