• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 8:55 PM
Mwanadada kila akilala anaota jinsi ‘ex’ alivyokuwa jogoo chumbani

Mwanadada kila akilala anaota jinsi ‘ex’ alivyokuwa jogoo chumbani

Na JANET KAVUNGA

BAMBURI, MOMBASA

MWANADADA wa hapa anaishi kwa wasiwasi kwamba huenda ndoa yake ikavunjika kufuatia ndoto zake akiwa na mpenzi wake wa zamani.

Hofu ya mwanadada ni kuwa, huwa anazungumza wakati wa ndoto hizo akimweleza ex wake anavyompenda wakiwa katika kilele cha burudani faraghani.

“Nakisia mume wangu amesikia nikizungumza kwa ndoto nikifurahia jinsi ex wangu alivyokuwa akinipagawisha. Sijui kwa nini ndoto hizi zinanijia kwa kuwa imepita miaka tangu nimuone ex wangu,” mwanadada alieleza.

Demu alikuwa akiongea na mashoga zake wakiwa saluni. Wenzake walimfariji na kumtaka atie bidii kujenga uhusiano wake na mumewe hasa katika masuala ya chumbani ili akome kumuota ex wake.

  • Tags

You can share this post!

Wakenya wamtarajia Rais kuangazia shida zao akituhubia...

Kawira roho mkononi akisulubiwa kwa mara ya pili Seneti

T L