NA JOHN MUSYOKI
ISINYA, KAJIADO
MTUMISHI wa Mungu barobaro aliyealikwa kuhubiri eneo hili alipata pigo, watu walipomsuta kwa kujipigia debe ili kujipendekeza kwa wanawake.
Kwanza, mhubiri huyo alijitia taabani kwa kuvalia suti iliyombana sana na kuanika misuli iliyotuna na nyeti.
Kisha akasinya waliohudhuria mkutano huo wa injili kwa kutoa matamshi ya kudhalilisha wanaume, kitendo walichodai ni kujipendekeza kwa vipusa.
Jamaa alitumia muda mwingi kujishasha badala ya kuhubiri.
Ni hali iliyokera umati wakaanza kulalamika huku baadhi wakinyanyuka na kumfokea vikali.
“Ulikaribishwa kuhubiri sio kujishasha. Unajipendekeza kwa wanawake ili wakushangilie lakini sisi tunachotaka ni injili,” watu wakateta.
Ilibidi pasta huyo kunyang’anywa mikrofoni umati ulipoanza kuondoka mmoja baada ya mwingine.